What's Trending?

Labels

Ads

Friday, July 10, 2015

HAKUNA KUCHELEWA, MESSI KUANZA MAZOEZI CHAMAZI LEO HUU NDIO MSHAHARA WAKE

11737180_920557287983039_2068690925_n
Stori kubwa leo hii  ni aliyekuwa winga wa Simba SC, Ramadhan Singano ‘Messi’ kusaini mkataba wa miaka miwili katika klabu ya Azam fc, ikiwa ni siku mbili tu tangu TFF wavunje mkataba wake na Wekundu wa Msimbazi.
Messi amesaini mkataba mnono kwa dau la milioni 50 na atakuwa analipwa mshahara wa Milioni 2 kwa mwezi.
Kabla ya kuingia katika mgogoro wa kimkataba na Simba, Wekundu wa Msimbazi walitaka winga huyo asaini mkataba wa miaka miwili kwa dau la milioni 30 na mshahara wa milioni 1.5, lakini alikataa.

No comments:

Post a Comment