Klabu ya Ac Milan imethibitisha kumtimua kocha wake, Filippo Inzaghi baada ya kuwa na msimu mbaya katika ligi ya Serie A na nafasi yake inachukuliwa na Sinisa Mihajlovic.
Mihajlovic ambaye alikuwa kocha wa Sampdoria msimu uliopita, amesaini mkataba wa miaka miwili kukinoa kikosi hicho na atalipwa karibia paundi milioni 2.5 kwa msimu.
Licha ya kumtimua kocha huyo AC Milan wamempongeza kwa kazi yake aliyoifanya akiwa kwenye klabu hiyo.
Ac Milan chini ya Inzaghi imemaliza msimu uliopita ikiwa imeshika nafasi ya kumi ikijikusanyia 52, wakati Mrithi wake Sinisa alimaliza nafasy ya 7 akiwa na Sampdoria.
No comments:
Post a Comment