MSANII wa Bongo Fleva anayeshikilia Tuzo ya Mwanamuziki Bora Chipukizi wa Mwaka (KTMA), Baraka Andrew ‘Barakah da Prince’ amelamba shavu la kufanya kolabo za kimataifa na Jaguar kutoka Kenya pamoja na Patoranking wa Nigeria.
Akifunguka na Centre Spread, Barakah anayebamba na Ngoma ya Nivumilie aliyoshirikiana na Ruby kutoka Jumba la Kuibua Vipaji (THT) alisema kuwa mbali na ujio huu alioutoa hivi karibuni yupo mbioni kufanya kazi za kimataifa.
“Tuzo imenipa heshima kubwa mjini. Nipo katika harakati za mwisho kufanya ngoma na Patoranking na baada ya hapo menejimenti yangu itamalizana na Jaguar kisha mtanisikia nikiwa naye katika ngoma moja,” alisema Barakah
No comments:
Post a Comment