
kipekee ambayo nilibahatika kuifahamu kupitia blog fulani hivi. Hata hivyo, chapisho hilo ambalo lilisomwa na maelfu ya watu, lilikuwa katika lugha ya Kiingereza. Makala hii ni marudio ya chapisho hilo kwa lugha ya Kiswahili. Maelezo hayo yanatoka mdomoni mwa Dkt Mwele mwenyewe ila mie nimetafsiri tu kwa Kiswahili.




Kazi zangu za awali zilijumuisha kuchunguza uhusiano kati ya parasaiti wa eosinophilia na helminth. Pia nilichunguza matokeo ya majaribio ya maangamizi ya malaria katika maambukizi ya Bancroftian Filariasis. Pia nilifanya kazi na marehemu Profesa Chris Curtis kudhibiti mbu aina ya Culex katika mji wa Muheza kwa kutumia dawa za kuua wadudu za polystyrene beads.
Baadaye nilikwenda London, Uingereza kufanya Shahada ya Uzamili na ya Uzamifu katika Taasisi ya Magonjwa ya Kitropiki ya Chuo Kikuu cha London, ambapo nilifanyia kazi maambukizi ya filarial kwa paka. Paka hao walikuwa kwa ajili ya majaribio ya uchunguzi ambao ulikuwa muhimu kwa uelewa wa maambukizi ya filarial. Kazi niliyofanya ilikuwa kupata uelewa jinsi parasaiti wanavymudu kukwepa mfumo wa kinga ya mwili wa kiumbe aliyeambukizwa, na matokeo ya uchunguzi wangu yaligundua kuwa kuna molekyuli za kiprotini (immunoglobulins) ambazo zilikuwa zikiwakinga parasaiti husika. Hii ilisaidia kuongoza uelewa kuhusu watu wenye maambukizi ya filarial lakini hawaonyeshi dalili za wazi.
Baada ya kurudi nyumbani, nilijihusisha na kuandaa utafiti wa kuelewa kitu ambacho kwa lugha ya kitaalam kinachoitwa immunoepidemiology ya maambukizi ya ugonjwa wa mabusha.Utafiti huo uliofanyika Kingwende, Kenya na Masaika, Tanzania. Machapisho kadhaa ya kitaaluma yalitokana na utafiti huo uliotuwezesha kufahamu zaidi kuhusu maambukizi ya ugonjwa wa mabusha, ambao ungetuwezesha kutafuta mbinu bora za udhibiti.

Wakati huohuo, nilihusika na kuandaa mpango wa kimkakati kwa ajili ya mradi wa kutokomeza mabusha nchini Tanzania. Hii ilifuatiwa na azimio la Shirika la Afya Duniani Mei 1997 ambalo lilisisitiza kuangamizwa kwa ugonjwa huo.Uaandaji wa mpango huo madhubuti ulifuatiwa na kuteuliwa kwangu kubwa mkurugenzi wa mradi unaohusu maradhi hayo mwaka 2000. Mwaka huohuo, mradi wa kupambana na ugonjwa wa mabusha ulianzishwa katika kisiwa cha Mafia, na mchango wangu kutoka maabara hadi kwenye eneo ambapo utafiti unatafsiriwa kwa vitendo ulitimia kamili. Kuna msemo wa Kiswahili kwamba safari moja huanzisha nyingine. Kwa upande wangu, hakujawa na mwisho wa safari hii bali ni vituo tofauti tu ninaposimama kidogo lakini naendelea mwelekeo huohuo.
Mradi huo wa kukabiliana na ugonjwa wa mabusha ulizidi kuimarika na sasa unafanya kazi katika wilaya 53 na umewafikia watu MILIONI 13. Huku msukumo sasa ukiwa kwenye magonjwa ya kitropiki yaliyosahaulika, njia zilizotumika katika mpango wa kukabiliana na ugonjwa wa mabusha zimepanuliwa na kujumuisha ugonjwa wa kichocho, minyoo wanaosambaa kupitia udongo na trakoma. Kwa kiasi kikubwa, usaili wangu katika makao makuu ya NIMR uliniandaa kwa ajira ya utafiti na udhibiti wa ugonjwa wa mabusha lakini kama ilivyo katika maeneo mengine ya maisha, sikujua hilo kwa wakati huo. Nilipata fahari kubwa pale Rais Jakaya Kikwete alipotangaza kuwa ataanzisha mfuko maalum kwa ajili ya ugonjwa huo kuwasaidia watu wanaosumbuliwa nao. Rais alitoa tangazo hilo katika Mkutano wa kimataifa wa masuala ya afya jijini Arusha, na hii imesaidia kupanua uelewa wa madhila yanayowakabili wahanga wa ugonjwa huo nchini Tanzania na kwingineko barani Afrika. Matokeo kutoka kituo cha uangalizi Tandahimba yanaonyesha mradi wa kukabiliana na ugonjwa wa mabusha umefanikiwa kupunguza maambukizi katika wilaya hiyo, na hiyo itakuwa sehemu ya kwanza ya mafanikio ya kuingilia kati maambukizi kwa upande wa Tanzania Bara.
![[IMG_7940.jpg]](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgNalvM7JflYJdTYZk5T5wy-wJZ7piHRJP5laPjV-5UNF2B31PqRGXy4jM-wwgMp2Z7m3v6cBXijt8eQpfx11Qp2ldK4ko-8RclQzYeOdnSW31DMoI4rCiCYsi30kSXZHnNXZ5jBHm0ue45/s1600/IMG_7940.jpg)
Je hii habari inayoelezea mafanikio? Ni habari kuhusu binti mdogo aliyekuwa na ndoto za kuwa mtafiti; kuhusu msichana aliyepanda vilima vya Amani kusaka ndoto yake, na ya mwanamke ambaye sasa anaishi katika ndoto hiyo kwa kufanya tafiti na kuchangia katika kukabiliana na ugonjwa ambao amekuwa akijishughulisha nao kwa takriban maisha yake yote. Labda hayo ndio mafanikio. Au waonaje?
Nina deni kubwa kwa watu wengi walioniwezesha kufanikisha safari hii, hususan baba yangu Dokta John Malecela na marehemu Mrs Ezerina Malecela ambao walinihakikikisha kuwa "ndiyo, waweza kutimiza ndoto yako."
Hapa chini ni machapisho mbalimbali ya kitaaluma
Malecela M.N. Baldwin C.I and Denham D.A (1994) Hosts antigen on the surface of microfilariae of Wuchereria bancrofti and Brugia pahangi.
Transactions
Awarded prize for best presentation
Baldwin C.I., Medieros F, Malecela M.N. and Denham D.A (1994) Humoral responses in cats repeatedly infected with Brugia pahangi. Parasite 1,1S
Malecela (1995): Microfilariae and the immune response in cats repeatedly infected with Brugia pahangi. Ph.D. thesis, University of London.
P.E.Simonsen, D.W Meyrowitsch, W.G.Jaoko,M.N.Malecela, D.Mukoko, E.M.Pedersen, J.H. Ouma, R.T.Rwegoshora, N.Masese, P.Magnussen, B.B.A Estambale and E.Michael (2001) Bancroftian Filariasis infection,Diseaese and Specific Antibody Response Patterns in a high and a low endemicity community in East Africa. Parasite Immunology 23: 373-388
Michael E., Simonsen P.E., Malecela M., Mukoko D., Pedersen E.M., Rwegoshora R.T., Meyrowitsch D.W, Jaoko W.G., (2001)Transmission intensity and immunoepidemiology of bancroftian filariasis in East Africa. Parasite Immunology No 23. Pp 373-388
Paul Simonsen,Peter Bernhard, Walter Jaoko, Dan Meyerowitsch, Mwele N.Malecela-Lazaro, Pascal Magnussen and Edwin Michael (2002) Filaria Dance sign and subclinical hydrocele in two East African communities with Bancroftian filariasis. Transactions of the Royal Society of Tropical Medicine and Hygiene
Simonsen,P.E, Meyerowitsch, D.W, Jaoko W.G., Malecela, M.N., Mukoko, D., Pedersen, E.M., Ouma,J.H., Rwegoshora, R.T., Masese.N Magnussen, P., Estambale, B.B.A & Michael E. (2002) Bancroftian filariasis infection disease and specific antibody responses patterns in a high and low endemicity community in East Africa. American Journal of Tropical Medicine and Hygiene Vol 66(5) pp550-559
No comments:
Post a Comment